TCRA NA TBN WATETA JUU YA ADA ZA USAJILI WA BLOGU MBALIMBALI

 
Viongozi waliokutana na Mhandisi  Andrew Kisaka  uliongozwa na Katibu Mtendaji wa TBN Khadija Kalili ,Kaimu Mwenyekiti TBN Rwehabura Rugambwa   ,Mweka Hazina Beda Msimbe  na Wajumbe  Muhidin Issa Michuzi, Frank Wandiba, Carren Mgonja na Shaaban Lulela . 
Mamlaka ya wasiliano Tanzania (TCRA) leo tarehe 19.03.2025 imekutana na na Uongozi wa Tanzania Bloggers Netwark (TBN) katika Ofisi za TCRA Makao Makuu Jijini Dar Es Salaam.

Na Mwandishi  Wetu 

Katika kikao hicho TBN imeiomba TCRA kupunguza gharama za usajili wa Blogs kama siuo kuziondoa kabisa.

Aidha TBN imeiomba TCRA iwe inatoa mafunzo ya mara kwa mara kwa Bloggers ilikuwajengea uzoefu katika kazi zao za kila siku.

Baada ya kusikiliza maombi hayo  Meneja wa Huduma za Utangazaji  TCRA Mhandisi Andrew Kisaka amesema wameyapokea maombi ya TBN na watayafanyia kazi huku ameahidi kutoa mrejesho.

Mhandisi  Kisaka ambaye ndiye alikua mwenyeji wa msafara huo wa Viongozi  wa TBN  amesema kuwa kwa niaba ya TCRA,

Mhandisi Andrew Kisaka akifafanua jambo mbele ya kamati ya Uongozi TBN iliyofika ofisini kwake leo  tarehe 19.Machi.2025 Jijini Dar es Salaam. 
 "Tunafurahi kukutana nanyi leo na kujadiliana mambo mbalimbali sambamba na kutambua namna mnavyoendesha shughuli za kihabari maana Bloggers mna umuhimu mkubwa sana kwenye maudhui ya ndani na kwa mustakabali wa nchi kwa ujumla hivyo ninawaahidi kuwa tumepokea maombi yenu, tutayanyia kazi na majibu tutawapatia" amesema Mhandisi Kisaka.

About life goes on

Blogger | Journalist | Entrepreneur | Fashonista Based in Dar es Salaam, Tanzania.

0 comentários :

Post a Comment

Copyright (c) 2024 LIFE GOES ON All Right Reserved

Developed by Gadiola Emanuel | 0784 643 633