DASH COMMUNICATION

DASH COMMUNICATION

ZANELLE BONGO LADIES WEAR

ZANELLE BONGO LADIES WEAR

ANDY BEACH

ANDY BEACH

AK

AK

NASAROG

NASAROG

NAKEMEA MAUAJI YA ALBINO

NAKEMEA MAUAJI YA ALBINO

Baby shop

Baby shop

COCO BEACH

COCO BEACH

RJ

RJ

PSSSF NA NSSF WAWASOGEZEA HUDUMA WANACHAMA WA MIFUKO HIYO KATIKA JENGO NAMBA 13 VIWANJA VYA MAONESHO SABASABA 2019

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) wamewasogezea karibu huduma Wanachama wa Mifuko hiyo katika msimu huu wa Maonesho ya 43 ya Bishara ya Kimataifa ya Dar es Salaam maarufu Sabasaba.




Wakizungumza leo Julai 2, 2019 kwa nyakati tofauti Wakurugenzi Wakuu wa Mifuko hiyo, Bw. Hoseah E. Kashimba (PSSSF) na Bw. William Erio (NSSF) wamesema kuwa wameamua kufanya maonesho hayo kwa kushrikiana ili kuwarahisishia Wanachama kupata huduma wanazohitaji wote wakiwa kwenye banda  namba 13 lililo mkabala na jingo la matangazo ndani ya viwanja vya Sabasaba.
“Tukiwa katika banda hili kwa kushirikiana na wenzetu wa NSSF ambao wao wanashughulika na wafanyakazi kutoka Sekta Binafsi na sisi PSSSF tunahudumia wafanyakazi kutoka Sekta ya Umma.”
 Tumeona tufanye maonesho haya pamoja kwa sababu ya kutoa elimu kwa wanachama kwa urahisi zaidi hasa kwa vile hatuko katika ushindani kama ilivyokuwa hapo awali, hii itasaidia kama Mwanachama anataka kujua taarifa kuhusu Mafao yake kama anatoka Sekta binafsi ataelekezwa aende NSSF na kama anatoka Sekta ya Umma ataelekezwa aende PSSSF, amefafanua Bw. Kashimba.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Bw. William Erio alisema “Baada ya kuunganishwa Mifuko hapo mwaka jana bado watu hawajaelewa vema tofauti zilizopo kwa hiyo wanakuja hapa kama banda pekee linalotoa huduma ya Hifadhi ya Jamii na wakifika basi wanaelekezwa katika sehemu husika na kupata huduma wanayohitaji.” Alisisitiza Bw. Erio.

Alisema ni sehemu ambayo watu wanaweza kuja na kujibiwa maswali yote waliyonayo na kutatuliwa kero zao.
Maonesho hayo ya kila mwaka yamefunhguliwa rasmi leo Julai 2, 2019 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan na yanatarajiwa kufikia kilele Jlai 13, 2019.
 Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF Bw. Hoseah E. Kashimba (wapili kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. William Erio (wapili kushoto) wakiwa na Mameneja Kiongozi Uhusiano na Elimu Kwa Umma, Bi. Eunice Chiume (kushoto) ambaye yuko PSSSF na Bi. Lulu Mengele (kulia) ambaye yuko NSSF.
Bw. Erio (kushoto) na Bw. Kashimba wakibadilishana mawazo ndani ya banda hilo.


 Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Bw. Hoseah E. Kashimba, (kushoto), akimuhudumia Mwanachama wa Mfuko huo aliyetembelea banda namba 13 la Mfuko huo na ule wa NSSF.

Picha ya pamoja ya wafanyakazi wa PSSSF na NSSF katika banda namba 13 viwanja vya Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam.

Life Life Life

Life is so beautiful,
Life is a game that you need to play if you win yeah that's good for you and if you loose your lost.
In life you need to have a shoulder to lay on, A friend is something important in life.
It's not easy to entertain people surround you all you need to do is praying and play well on your line.
To have a friend is something so sweet and you need to enjoy every moment with you're truly one and if comes the time you feel pain or sweet moment turns to hard and tough moment ohooo babe you need to quite the friendship although definition of truly friendship is giving all without expecting back.
Life Goes On is encourage you to keep your friendship and leave a happy life.

Life Goes On........................

PINGA UKATILI WA WANAWAKE TANZANIA

Mpaka karne hii bado mila potofu zinaendelea kutumika katika jamii, mila ambazo zinaendelea kuwanyanyasa kijinsia wanawake na kuwafanya wajione sio kitu katika jamii.


Mapema mwezi April nilipata fursa ya kuambatana na shirika la kivulini mjini Tarime tukiwa chini ya ufadhili wa Oxfam Tanzania na kuzungukia mikoa ya Mara hii ni pamoja na Shinyanga, Mwanza, Musoma Tarime na Butihama.
Huko tulikutana na changamoto nyingi wanazopitia wakina mama na watoto bila ya kuwa na msaada wowote katika jamii au serikalini.


Picha ya Judy Mwaheleja
Mzee wa mila Tarime pichani ambaye mwenye nyazifa ya uwenyekiti wa mila akithibitisha ukeketaji kwa mabinti wadogo unaendelea kijijini hapo ili kudumisha mila mwanamke akiolewa atulie na mume mmoja.


Wazee wa kijiji ambao ndio wana madaraka ya shughuli za kimila na ambao wanaheshimiwa hawajaweza kuwa msaada kwa wamama hawa na mabinti kwani bado sehemu kubwa ya tarime wanaendeleza mila hizo potofu kwa manufaa yao binafsi ya kujipatia kipato. Walituhoji wakiacha hiyo mila watakula wapi?


Tumegundua ukeketaji wa mabinti wadogo umekithiri na kupelekea watoto kufariki katika zoezi hilo kwani hawatumii njia sahihi za kuwakata maumbile yao na kuwapelekea kupoteza damu nyingi sana wakati mwingine inawapelekea kupata Vistula hapo baadae.
Kipindi cha ukeketaji watoto wa kike wanachukuliwa na kupelekwa maporini hii inawapotezea vipindi vya masomo yao na kushindwa kufanya mitihani yao vizuri
Kwakweli tumeona kabisa hamna msaada kwa mabinti hawa kwasababu mama zao hawana sauti katika familia na hata wakienda kushitaki polisi wanaambiwa ni mgogoro wakifamilia warudi waelewane kifamilia na hata wakiwakimbilia wazee wa kijiji huko ndiko wanakamatwa kabisaa na kufanyiwa vitendo hivyo kwani hawa wazee wa mila ndio biashara yao na wanajipatia riziki kwa kupitia shughuli hii. Kwa binti mmoja akikeketwa wanalipwa sh 25 elfu tunaona hapo ina sababisha kuwa vigumu kuangamiza vitendo hivyo vya kiukatili.
Makabila mengi ya Mara mwanamke kupigwa adharani hadi kuvuliwa nguo hiyo ndio sifa ya baba kuwa na yeye ni mume
Uzalilishaji wa kukeketwa mabinti umekithiri yote hayo wakiamini wanadumisha mila ili wazazi waweze kupata ng'ombe wengi maana mabinti watatulia hadi siku watakapo olewa, kwao lengo kwa mtoto wa kike si elimu au aje kuwa kiongozi Fulani au daktari wenyewe wanawaza atafikisha lini miaka 15 ili aweze kuolewa na kipindi hicho cha kuolewa kwakwe ng'ombe wangapi atapata.
Unyanyasaji unaendelea mpaka kwa mama mtoto maana baba anachukua mtaji wa ng'ombe wa mtoto wa kike aliyemuozesha na yeye anaenda kuongeza kuoa mke wapili ambapo analeta uadui kati ya wake zake. Hakuna atakaye furahia mahali ya mwanae halafu unaenda kuniolea mke mwingine! kwakweli hali inasikitisha.


Picha ya Judy Mwaheleja
Nikiwapa elimu mabinti watambue haki zao za msingi ikumbukwe kuwa Ukatili Sio Jibu project hii ilikuwa chini ya uzamini wa Oxfam Tanzania.


Tuliweza kuwaita wazee wa mila na kuwapa elimu ya umuhimu wa haki za wanawake akiwemo Mwenyekiti wa mila, Askari polisi dawati la jinsia, Diwani wa halmashauri ya Tarime na wananchi mbali mbali waliokumbwa na janga na wengine walio shuhudia vitendo hivyo vya kikatili. Lakini tukagundua sisi pekee haitatosha kukabiliana na matatizo wanayokumbana nayo wanawake na mabinti wa mikoa ya Mara.
Picha ya Judy Mwaheleja


Basi nini kifanyike ili kutokomeza hali hiyo?
Kwanza wazee wa mila waangaliwe na wawezeshwe kiuchumi ili nazani litafanyiwa kazi na diwani wa maeneo husika wataweza kuwasilisha taarifa kwenye ngazi za juu. Kwakufanya hivyo tutaweza kuwafanya wazee wa mila na wananchi wa maeneo kuwa na kauli moja ya HAPANA ukeketaji na udhalilishaji wa mwanamke. Kila mmoja atamlinda mwanamke.
Uthubutu kwa wahanga wa unyanyasaji kuweza kupaza sauti watakapo ona wanataka kutendewa vitendo vya ajabu. mfano kama mama anajua kuna mipango ya baba kumpeleka mtoto wa kike kukeketwa basi awajulishe jamii inayowazunguka kwapamoja waje wazuie.
Sheria nyingine zifanyiwe marekebisho ushahidi wa mahakamani uangaliwe upya mtu akishitaki amebakwa na mtu fulani basi ripoti ya daktari ikidhibitisha mshatakiwa apewe athabu kali na sio unamwambia mtu leta shahidi sasa shahidi atamtoa wapi wakati vipimovina sema kafanyiwa ukatili fulani na anakuambia ni huyu. Watuhumiwa wasipochukuliwa hatua wanarudi kulipa kisasi na kuwafanya wengine waogope kupaza sauti.







WORLD SHOULD KNOW HOW IMPORTANT OF WOMEN

Woman are flowers are sweet mama's that every one need to have a side.
are good shoulder when we cry good hands when we need support and good advisers.

Woman can do well cooking, washing, cleaning than man, they do well domestic tasks, and making the home a healthier, safer and more comfortable place we need to thanks them.

And when we empowering a woman you will help all societies because, if woman do things always did for the family benefit or society deferent with man he can spend on his own without caring the family.

Woman are not for kitchen only......
Help woman to get education and to be leaders this will help societies to have equal gender. Women can be better leaders and bring better and peaceful country or society give them chances.



STOP POVERT IN THE WORLD

I am a woman with two kids. I never experience poorness in my life. I only read this in magazine and watch in news.
My parents works in Government so we got all basic needs.
Now I have my life on my own and parents are old and retired .
I found out poverty can happen any time to anybody if you wont take action of fighting it.
Poverty is not for African people only is for anybody this is why awareness is needed that we can prevent it.
Image result for poor people



How can we fight for poverty?
We can introduce projects to young's in certain villages or societies
We can improve peoples famers and other works or sells to enable them to depend on their own.
By empowering women because woman can lift their families out from poverty

Image result for poor people

World!!!! let share here means to STOP POVERTY IN THE WORLD and let's do necessary action.
contact me on my mail jeedygal@gmail.com or phone me on +255658021981 or WhatsApp on same number.











TUMIA VYEMA MITANDAO YA KIJAMII

 

Mimi nashiriki kampaini ya kusisitiza matumizi bora ya mitandao ya kijamii wewe je?

Kama hujachukua hatua fanya sasa kuepuka vyombo vya dola sheria ipo na inafanyiwa kazi trust me

TOP BEAUTIFUL WOMEN IN TANZANIA

WEMA SEPETU
Image result for wema sepetu 2017
Related image
Related image
Related image


NANCY SUMARI
Related image 

Image result for nancy sumari 
Image result for nancy sumari 

ELIZABETH LULU MICHAEL
Image result for elizabeth michael lulu 
Image result for elizabeth michael lulu 
Related image 
Related image

JACKLINE WOLPER
Image result for jackline wolper 
Image result for jackline wolper 
Image result for jackline wolper 
Related image 

HAMISA MOBETO
Image result for hamisa mobeto 
 Image result for hamisa mobeto 
Image result for hamisa mobeto
Image result for hamisa mobeto 

AGNESS MASOGANGE
Related image
Image result for Agness masogange 
Image result for Agness masogange 
Image result for Agness masogange 

IRENE UWOYA
Related image
Image result for irene uwoya 
Image result for irene uwoya 
Related image 
Related image 
Image result for irene uwoya 2017 
.....................TO BE CONTINUED......


TCRA YASHIRIKIANA NA BLOGGERS KUSISITIZA MATUMIZI BORA YA MITANDAO YA JAMII




 Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Jones Kilimbe akifungua rasmi warsha ya vyombo vya Habari Mtandaoni iliyo wahusisha Blogu na 'Online Tv' katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa J.K Nyerere Jijini Dar es salaam.
 Bw. Thadeus Lingo kutoka TCRA akiendesha mada kuhusu Matumizi Salama ya Mitandao ya Kijamii
 Mwakilishi wa Chama cha wamiliki wa Blogu Tanzania(TBN) Bw. Maxence Melo akiwasilisha mada juu ya Maudhui ya Mtandaoni na Changamoto zake.
 Mratibu Msaidizi wa Polisi Joshua Mwangasa akitoa mada juu ya Hali ya Usalama Mtandaoni

 Mzee Abdul Ngarawa Mjumbe wa Kamati ya Maudhui kutoka TCRA akitoa neno la Busara wakati wa warsha hiyo ambapo alisisitiza kuzingatia uzalendo umuhimu wa kutazama utu na staha ya mtu

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi James Kilaba (Kushoto) akiongoza majadiliano kwa ujumla ambapo wadau walichangia mawazo na kuuliza maswali mbalimbali

Bwana Daniel Mbega Mmiliki wa Blogu ya Maendeleo Vijijini akichangia mawazo yake wakati wa warsha hiyo

 Bw. William Malecela Maarufu kwa jina la Le Mutuz mmiliki  Blogu ya Wananchi na Le Mutuz Tv Onine akichangia mambo mbalimbali na kutoa maoni yake wakati wa Warsha hiyo

 Mwenyekiti wa  Chama cha wamiliki wa Blogu Tanzania(TBN) Bw. Joachim Mushi (kulia) akitoa neno la Shukurani kwa niaba ya waendesha wote wa mitandao kwa TCRA kuendesha warsha hiyo

  Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi James Kilaba pamoja na wadau wengine wakizindua Rasmi Kampeni ya kusisitiza matumizi bora ya Mitandao ya Kijamii awamu ya Pili ambapo Kauli mbiu inasema "Usinitumie Sitaki na Simtumii Mwengine Nitakuripoti"

 Baada ya uzinduzi wa Kampeni hiyo.

 Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya TCRA Bi. ValerieNdeneingo-Sia Msoka akitoa neno la kufunga wakati wa Warsha hiyo.


 Wadau mbalimbali wakiwa katika warsha hiyo



 
Serikali ya Awamu ya Tano kupitia Mamlaka ya Mawasiliano nchini(TCRA) imetia nia kuboresha mawasiliano kwa umma hasa katika matumizi ya mitandao ya kijamii ili kuwawezesha watanzania kupata elimu bora ya maendeleo na kujenga uchumi uliobora.

Haya yamesemwa katika kampaini ya kusisitiza kutumia matumizi bora ya mitandao ya jamii jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Bodi wa Mamlaka hiyo Dkt. Jonas Kilimbe  alipokua akihutubia hadhara ya wamiliki wa vyombo vya habari mtandaoni (blogu na Online TV) katika uzinduzi wa kampeni ya awamu ya pili ya “kusisitiza matumizi bora ya mitandao ya kijamii”  iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere.

Katika hafla hiyo, Dkt. Kilimbe alisema kuwa kwa sasa teknolojia ya mtandao inakua kwa kasi kwa hiyo huduma za habari zinapatikana kila sehemu kwa njia ya mtandao na kufanya matumizi ya mitandao kuwa makubwa.

“Sekta ya mawasiliano kwa umma imepiga hatua kubwa sana duniani kwa sasa, kwa kiasi kikubwa mtandao unachangia kuwepo kwa habari nyingi. Tanzania inajumla ya televisheni za mitadaoni zipatazo 50 pamoja na blogu 150 ambazo zote zinatoa taarifa kwa wananchi, hii inaashiria kuwa mawasiliano kwa umma yamehamia zaidi kwenye mtandao”, alisema Dkt.Kilimbe.

Aidha Dkt.Kilimbe alisema kuwa sekta hii inapaswa kuangaliwa zaidi kwani ni sekta muhimu kwa ujenzi wa Taifa na kuwaasa vijana kutumia vizuri teknolojia hiyo kwa kujielimisha kuhusiana na masuala ya maendeleo kuliko kutumia vibaya mitandao hiyo.

“Tuna jukumu zito na ni kubwa kwa sababu sekta hii ya mawasiliano imeshikiria kila kitu na tasnia ya habari ina nguvu kubwa sana kwa kuleta elimu ya maendeleo kwa wananchi kwa hiyo waandishi mitandaoni tumieni weledi  mkubwa kwa habari za maendeleo.”, alisisitiza Dkt. Kilimbe.
Dkt.Kilimbe alisema kuwa katika matumizi ya teknolojia hii mpya yanapaswa kuzingatiwa  kwa ajili ya ujenzi wa taifa hasa kwa wale wanaotumia vizuri mitandao ya kijamii inawapa elimu kubwa ya maendeleo.

Aidha Dkt. Kilimbe amekishukuru chama cha wamiliki wa blogu na televisheni mtandaoni(TBN) kwa kuleta umoja na kuzingatia maadili na weledi wa umilikajia wa vyombo hivyo kwa kuwahabarisha wananchi.

Naye mtoa mada na mwakilishi kutoka TCRA Bw. Thadeus Lingo alisisitiza usalama wa matumizi ya mtandao akisema kuwa idadi ya watumiaji wa mitandao imeongezeka duniani kuanzia Julai 1, 2017 na kufikia bilioni 3.8 huku kati ya hao bilioni 3.4 ambayo ni sawa na asilimia 92 ni watumiajia wa mitandao ya kijamii hali iliyosababisha kuongezeka kwa vyombo vya habari kuhamia mtandaoni, kwa hiyo weledi unahitajika katika kuhabarisha umma kwa njia hii.
Picha ya Judy Mwaheleja
Life Goes On Blog ilifanikiwa kushiriki katika halfa hiyo ya kampeni ya kusisitiza kutumia matumizi bora ya mitandao ya kijamii.
 

 
Supported by : Jeedy Girl
Copyright © 2012. life goes on - All Rights Reserved
Modified by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Jeedy Girl