DASH COMMUNICATION

DASH COMMUNICATION

ZANELLE BONGO LADIES WEAR

ZANELLE BONGO LADIES WEAR

ANDY BEACH

ANDY BEACH

AK

AK

NASAROG

NASAROG

NAKEMEA MAUAJI YA ALBINO

NAKEMEA MAUAJI YA ALBINO

Baby shop

Baby shop

COCO BEACH

COCO BEACH

RJ

RJ

Home » » WAFANYAKAZI WA MGODI WA BUZWAGI WASHEREKEA SIKU YA FAMILIA NA FAMILIA ZAO

WAFANYAKAZI WA MGODI WA BUZWAGI WASHEREKEA SIKU YA FAMILIA NA FAMILIA ZAO

Eng.Philbert Rweyemamu akifafanua jambo katika moja ya mabanda ya maonyesho kwa baadhi ya maafisa wa uhamiaji walipokuwa wakitembelea mabanda ya maonyesho.
Eng.Philbert Rweyemamu akifafanua jambo katika moja ya mabanda ya maonyesho.
Wageni wakijionea namna mradi wa matofali ya gharama nafuu ulivyowanufaisha wenyeji wanaozunguka mgodi wa Buzwagi.
Wageni wakipata maelezo kutoka kwa wataalamu wa kampuni ya KALTIRE ambayo imekuwa ikihudumia mgodi wa Buzwagi kwa kuwauzia matairi kwa ajili ya mitambo ya uchimbaji mgodini hapo.
Wageni pamoja na baadhi ya maafisa wa mgodi wa Buzwagi na wale wa serikalini wakijionea matairi makubwa yanayotumika katika mgodi huo.
Wageni wakipata maelezo wakati walipotembelea banda la PANAF
Sehemu ya familia za wafanyakazi wa mgodi wa Buzwagi wakiwa wameketi baada ya kutembelea mabanda mbalimbali
Kama vile hawaamini!!!! Ni kweli anacheza na nyoka hivyo?
Kuhakikisha kumbukumbu hii haipotei kamera za simu zikafanya kazi yake
Kikundi hiki cha Ngoma kutoka Shinyanga kilitia fola kwa burudani safi ya Ngoma waliyoitoa.
Baadhi ya maafisa wakuu wa kampuni ya Acacia wakifuatilia burudani ya ngoma
Michel Ash-Afisa Mkuu wa Masuala ya uendeshaji wa kampuni ya Acacia akizungumza na familia pamoja na wafanyakazi wa mgodi wa Buzwagi
Baadhi ya maafisa wa idara ya ufanisi wa Mgodi wa Buzwagi wakiwa katika picha ya pamoja katika banda lao wakati wa maonyesho
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi mwenye shati la bluu akiongozwa na mkuu wa kitengo cha ulinzi Jamal Rwambol kutembelea mabanda ya maonyesho
Azael Kitange-Mkufunzi wa idara ya ufanisi wa kampuni akitoa maelezo kwa wageni walipotembelea banda la idara ya Ufanisi katika kitengo cha Mafunzo.
Ufugali wa nyuki wa kisasa ni moja kati ya shughuli zinazofanywa na mgodi wa Buzwagi kupitia idara ya Mahusiano ya Jamii kwa kuwawezesha wenyeji wanaozunguka maeneo ya mgodi kujipatia shughuli zinazowaongezea kipato.
Wataalamu wa idara ya afya wakionyesha baadhi ya vifaa mbalimbali vinavyotumika kupima afya za wafanyakazi wakati wote ili kuhakikisha afya za wafanyakazi wa mgodi huo muda wote zinakuwa salama.
Wataalamu wa miamba wakionyesha aina mbalimbali za miamba yenye dhahabu na namna wanavyotumia vifaa vya kisasa kuitafuta dhahabu.
Kikundi cha Ngoma cha kabila la wasukuma kikitoa burudani ya ngoma wakati wa maadhimisho ya siku ya familia kwa wafanyakazi wa mgodi wa Buzwagi
Baadhi ya wanafamilia wa wafanyakazi wa mgodi wa Buzwagi.
Baadhi ya maafisa kutoka Mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu wakifurahia moja ya burudani wakati wa sherehe hizo.
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Eng. Philbert Rweyemamu (katikati) na Meneja wa Biashara wa Mgodi huo wakifuatilia kwa makini burudani zilizokuwa zikiendelea wakati wa sherehe hizo, kushoto kwao ni mwakilishi wa Mkuu wa wilaya ya Kahama.

Meneja Ufanisi wa Mgodi wa Buzwagi Bwana Saimon Sanga akizungumza na wafanyakazi wa Mgodi huo wakati alipokuwa akimkaribisha meneja Mkuu wa mgodi wa Buzwagi.
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Eng.Philbert Rweyemamu akizungumza na wafanyakazi wa Mgodi huo pamoja na familia zao wakati wa sherehe za siku ya familia.
Watoto wakishiriki michezo mbalimbali iliyokuwepo maalum kwa ajili yao
Watoto wakishiriki michezo wakati wa sherehe hizo.

Graham Crew-Meneja Mkuu wa Mgodi wa Bulyanhulu (kushoto) akiteta jambo na Michelle Ash-Afisa Mkuu wa masuala ya uendeshaji wa kampuni ya Acacia wakati wa sherehe hiyo
Mtaalamu wa masuala ya uchimbaji wa Mgodi wa Buzwagi akitoa maelezo kwa wageni waliotembelea banda la idara yake.
Mmoja wa wafanyakazi wa wa Idara ya masuala ya usalama wa Mgodi wa Buzwagi akitoa maelezo kwa baadhi ya familia za watumishi wa mgodi huo wakati walipo tembelea banda maalum la maonyesho la idara ya usalama mgodini.
Mmoja wa wafanyakazi wa mgodi wa Buzwagi Bwana Moses Msofe akiwa na familia yake kusherekea siku ya familia
Wazazi wakiwasimamia watoto wao walipokuwa wakishiriki michezo mbalimbali ya watoto.
Watoto wa baadhi ya wafanyakazi wa Mgodi huo wakifurahia michezo mbalimbali wakati walipokuwa wakiadhimisha siku ya familia mgodini hapo
Baadhi ya ndugu wa wafanyakazi wa Mgodi wa Buzwagi wakiangalia aina mbalimbali za mashine zinazotumika katika shughuli za uchimbaji katika mgodi huo.
Moja kati ya magari makubwa kabisa yanayotumika katika mgodi huo likiwa katika eneo la maonyesho.
Kutoka kushoto ni meneja wa uendelezaji wa Mgodi wa Buzwagi George Mkanda, katikati ni Graham Crew-Meneja Mkuu wa Mgodi wa Bulyanhulu na  Michelle Ash-Afisa Mkuu wa masuala ya uendeshaji wa kampuni ya Acacia wakati wa sherehe za siku ya familia ya Mgodi wa Buzwagi.
Baadhi ya familia za watumishi wa Mgodi wa Buzwagi zikitambulishwa wakati wa hafla hiyo.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii aliyekuwa Kahama.

Buzwagi imeanzisha mkakati wa kukuza na kuboresha hali ya utendaji kazi kwa wafanyakazi wake kwa kuanzisha utaratibu wa kuwakutanisha wafanyakazi wa mgodi huo na familia zao mara moja kwa mwaka katika siku maalumu ya familia ambayo hutoa fursa kwa familia za wafanyakazi wa mgodi huo kuweza kujionea namna ambavyo shughuli za uchimbaji wa madini hufanyika na hivyo kuwa mabalozi wazuri wa kampuni kwa ujumla.
Mwaka huu wafanyakazi wa kampuni hiyo wamepata fursa ya kukutana na kujionea shughuli mbalimbali ambazo zimekuwa zikifanyika mgodi hapo. Pamoja na mambo mengine wafanyakazi hao pia walipata fursa ya kutembelea eneo ambapo shughuli za uchimbaji zinafanyika.
Sherehe hizo zilihudhuliwa na Afisa mkuu wa masuala ya uendeshaji  Michelle Ash, Meneja Mkuu wa Mgodi wa Bulyanhulur-Graham Crew na meneja mkuu wa masuala ya ufanisi wa kampuni Janet Ruben pamoja na meneja mahusiano na mawasiliano wa Acacia Nector Foya, pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali..

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by : Jeedy Girl
Copyright © 2012. life goes on - All Rights Reserved
Modified by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Jeedy Girl