JUST FLOWERS DAY 2020

Just Flowers Group ni kundi la wadada na wakaka wachache wapambanaji wapenda maua na wafanya biashara ya maua na vyombo vya kuhifadhia maua ikiwemo mbegu na dawa za kutunzia maua.

Kundi hilo limeanzishwa na dada kipenzi wa watu mpambanaji maarufu hapa nchini Tanzania Maza Sinare maarufu kwa jina la Maznat kutokana na Biashara zake za saluni na make up studio na maua hapa jijini Dar es salaam
Kiongozi huyo wa Just Flower alianzisha event hii na kuipachika jina la JUST FLOWERS DAY ikiwa moja ya kuunganisha wapenda maua pamoja na kuwasaidia kutangaza na kuuza biashara zao za maua na kuwapatia elimu kwa kuwaita wataalamu wa maua mbalimbali 


Pichani; Mwazilishaji wa JUST FLOWER Maznat akimgawia zawadi ya ua na dawa ya kuzuia wadudu kwenye maua muuza maua chipukizi Judith Mwaheleja kwenye sherehe hizo za JUST FLOWERS DAY 2020


Wana Just Flowers wakisherekea siku hiyo kwa furaha









Matukio mbalimbali ya siku hiyo iliyofana kama picha zinavyoonyesha ikiwemo kula kunywa mafunzo na kufanya biashara bila kusahau kuserebuka na zawadi juu
Kweli kujiunga JUST FLOWERS ni deal changamkia fursa mtafute Maznat mwenye Just Flowers yake hapa mjini.

 

About life goes on

Blogger | Journalist | Entrepreneur | Fashonista Based in Dar es Salaam, Tanzania.

0 comentários :

Post a Comment